Polisi Wazingira Ofisi za Upinzani, Bunge na Maeneo Muhimu ya Jiji la Kmpala

Polisi Wazingira Ofisi za Upinzani, Bunge na Maeneo Muhimu ya Jiji la Kmpala
Maofisa polisi wamesambazwa katika maeneo mengi muhimu katika jiji la Kampala ulinzi unaohusiana na mjadala juu ya pendekezo la kufutwa Ibara ya 102 (b) ya Katiba likilenga kuondoa ukomo wa umri wa rais.

Makao makuu ya ofisi za chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) kinachoongozwa na Dk Kiiza Besigye kuanzia jana yamezingirwa na polisi wa kawaida, wa kuzuia ghasi na wa kupambana na ugaidi. Ofisi hizo zilizopo Najjanankumbi katika barabara ya Kampala-Entebbe zimezungukwa na polisi wenye silaha.

Msemaji wa Polisi Asan Kasingye alisema jana kwamba maofisa hao wamesambazwa kwa ajili ya kukabiliana na kitisho cha aina yoyote. Kadhalika maeneo mengi nyeti, eneo lililojaa shughuli za kibiashara na Bunge yote yanalindwa.

Polisi wa kijeshi pia wamesambazwa maeneo ya Constitution Square ambako wameweka mahema sawa na bungeni, eneo muhimu kwa ajili ya mjadala unaotarajiwa kuwasilishwa leo kuhusu kuondolewa ukomo wa umri.

Kusambazwa kwa wingi kwa askari hao kumefanyika katikati ya kampeni zinazofanywa na za vikundi vya kisiasa na sasi za kiraia kupinga marekebisho ya katiba yanayolenga kufuta ukomo wa umri wa rais wa miaka 75. Hoja ya marekebisho hayo ilitarajiwa kuwasilishwa leo baada ya
kushindikana
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad