Shilole Adaiwa Kumtesa Mpenzi Wake Mpya Uchebe Kama Alivyokuwa Anamburuza Mziwanda

MKALI wa miondoko ya Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ anadaiwa kumtesa mpenzi wake, Ashiraf Uchebe na kwamba imefikia kipindi anamgombeza mbele za watu kama mtoto mdogo. Kwa mujibu wa chanzo, kiliitonya Star Mix kuwa, juzikati katika Ukumbi wa Maisha Basement, Kijitonyama jijini Dar, Shilole alionekana akimkoromea Uchebe.

“Yaani hadi aibu, Shilole sijui kwa nini aliamua kufanya vile, kuna wakati alikuwa akimnyooshea vidole na kumsuka,” kilisema chanzo kilichohudhuria ukumbini hapo.

Star Mix baada ya kuunyaka ubuyu huo, ilimvutia waya Shilole ambapo alisema; “Jamani watu wanajua kukuza mambo na kuniona kama mimi ni mkorofi kila wakati kwenye mapenzi, lakini siamini kabisa kwenye mapenzi hakuna ugomvi wala purukushani kwani vyote nisehemu ya mapenzi.”

Global

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. jitu ambalo halijasoma halijui dini si she can do anything anaona its fun but mbele ya watu yeye ni kama cartoon vichekesho hata kusikia j8na lake or to see her inakirihisha as a lady na hao wanaume wenye kungangania ni wajinga

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad