Simba Kujiweka Shinyanga kwa Maandalizi ya Mechi yao Dhidi ya Stand United

Simba Kujiweka Shinyanga kwa Maandalizi ya Mechi yao Dhidi ya Stand United
Klabu ya Simba leo inatarajiwa kutua mkoani Shinyanga kwaajili ya maandalizi ya mchezo wake wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara dhidi ya Stand United wiki ijayo.

Simba imeanza safari mapema leo kutokea Mwanza ambako ilicheza mchezo wake wa raundi ya nne dhidi ya Mbao FC ambao ulimalizika kwa sare ya 2-2.
Kwa upande mwingine msemaji wa Simba Haji Manara amethibitisha kuwa winga wa timu hiyo Shiza Kichuya anaendelea vizuri na atapumzika kwa simu 2 kuanzia leo kisha atakuwa fiti kwaajili ya mchezo dhidi ya Stand United.
Kichuya aliumia kipindi cha kwanza kwenye mchezo dhidi ya Mbao FC ikiwa ni baada tu ya kufunga bao lake la kwanza msimu huu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad