Trump Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Demokrat

Trump Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Demokrat
Rais wa Marekani Donald Trump amekutana na wanasiasa wawili waandamizi kutoka chama cha Demokrat katika bunge la Congress kujadili maswala tata, huku pande zote mbili zikisema mazungumzo hayo wakati wa chakula cha jioni ikulu ya white house yalikuwa yenye manufaa.
Katika taarifa, Chuck Schumer na Nancy Pelosi wamesema wamekubaliana kuunda mpango wa pamoja kuhusu usalama wa mipakani na Donald Trump.
Wanasema mpango huo unajumuisha kuwalinda wahamiaji wenye umri mdogo lakini haukujumuisha ujenzi wa ukuta kwenye mpaka na taifa la Mexico.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad