Tundu Lissu Apelekwa Nairobi Kwa Matibabu...Akodishiwa Ndege Binafsi

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ameondoka katika uwanja wa ndege wa Dodoma usiku wa leo kwenda Nairobi kwa ajili ya matibabu.

Lissu ambaye alijeruhiwa akiwa kwenye gari nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulika.

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini amesema, katika safari hiyo Lissu ameambatana na mkewe, madaktari wawili wasio na mipaka, Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Selasini amesema kuwa Lissu anapelekwa katika Hospitali ya Aga Khan mjini Nairobi.

Ndege hiyo iliyombeba ya 5H-ETG imeondoka katika Uwanja wa Dodoma saa sita na robo usiku.
 

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Bawicha inaelekea waujua mchongo wote ndani kwa ndani katika chama na tukio.
    Lazima wasaidie upelelezi

    ReplyDelete
  2. Lizu umetudhalilisha.
    Hii inadjihirisha ukozefu Wako WA imani kwa Madaktari wetu WA Kitanzania na vyombo tulivyonavyo katika fani ya Utabibu.
    Inaonesha kuwa posho kmekulevya na sisi walipa kodi guendelee na jjospiyali zetu na wewe ukimbilie huko nje kea ndege binafsi.
    Lakini hii yote I wewe ndiye yule yule mpaka huu wakati mgumu unaonesha hamba lako halibadiki.
    Sasa na kama kuzikea utazikiwa nje au...!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad