Video ya Fiesta Mwanza Yamtia Jirani Yangu Matatani..Anaswa Akijarusha na Mwanamke

Wakuu, leo kwa jirani yangu pamechimbika mke wake kaliamsha dude.

Wakuu mda so mrefu nimeingia kwangu nikitokea kuijenga Tanzania ya viwanda, ila baada ya kufika ndani nasikia kwa jirani yangu makonde mazito yanatembea huku matusi na kelele zikisindikiza mpambano huo wa aina yake ulionivutia niufatilie.

Baada ya kuona ugomvi huo kati ya jirani yangu na mkewe hauishi, nikaamua kuenda kusikiliza kipi kimewasibu ila kabla sijafika nikasikia mke anatukana huku anasema wewe uliaga umeenda lindo kumbe umeenda Fiesta maneno hayo yakanipa hamasa ya kufuatilia kulikoni, kufika pale nikagonga mlango kwa nguvu jamaa kafungua nikauliza vipi mbona mnauana jamaa akijiandaa kujibu mkewe akatoka ndani na kuanza kumshtakia mme wake kwangu.

"Shem rafiki yako aliondoka Jumamosi jioni akaniambia anaenda guard (lindo) alafu akarudi jpili asubuhi basi siku imepita sasa leo nikaamua niingie you tube ili kuona Fiesta mwanza ilikuwaje make sikuenda kwasababu sikuwa na kampani mke, mume wangu aliaga ameenda lindo, ila cha ajabu nikiwa naendelea kuangalia nkamuona mume wangu akiwa anashangilia huku kalibambia limalaya limoja lina mikalio kama Sarah Bahtman nimejisikia kuishiwa nguvu make mi aliniaga anaenda kazini kumbe anaenda fiesta Kirumba"

 Nb: Wakuu mkienda kwenye starehe ambazo unajua kuna mtu hutaki ajue uwepo wako pale epuka kuonekana kwenye mipicha na mavideo yanayochukuliwa na watu maana unaweza umbuliwa one day.

JF
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad