Vigogo Waliokamatwa na Almasi za Bilioni 32.3 Uwanja wa Ndege Wafikishwa Mahakamani Leo

Waliokamatwa na  Almasi Uwanja wa Ndege Wafikishwa Mahakamani Kisutu
Watuhumiwa waliokamatwa na mzigo wa almasi zenye thamani ya Sh 32.3 bilioni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA), wamefikishwa mahakamani Kisutu asubuhi leo Ijumaa.

Watuhumiwa hao walikamatwa na mzigo huo ambao ulizuliwa na Serikali ili ufanyiwe tathimini upya kujua thamani halisi baada ya thamani iliyotumika kutiliwa mashaka na Serikali.

Jeshi la polisi liliwashikilia watuhumiwa wanne kwa uchunguzi na hatua nyingine za kisheria baada ya kuzuia mzigo huo.

Mzigo huo wa almasi ulikuwa unatoka mgodi wa Mwadui ambao ni wa ubia kati ya Serikali na kampuni ya Petra Diamonds ya Afrika Kusini kwa hisa 25 za Serikali na Petra  Diamonds hisa 75.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad