Waziri wa Afya Ajiuzuru

Waziri wa Afya Ajiuzuru
Waziri wa afya nchini Marekani, Tom Price amejiuzulu baada ya kukodi ndege binasfi ikiwa ni kwa ajili ya shughuli za kiserikali.

Waziri Price aliomba radhi kwa kufanya safari akitumia ndege za kukodi mara 26 tangu mwezi May kwa gharama za dola za kimarekani 400,000 zikiwa ni fedha za walipa kodi nchini humo.
Nchini Marekani maafisa wa serikali isipokuwa wale wanaoshughulikia masuala ya usalama wanatakiwa kutumia ndege za abiria katika safari za kikazi. Habari zinasema mawaziri wengine watatu katika utawala wa Trump wanachunguzwa kwa kutumia ndege binafsi za kukodi kwa shughuli za serikali.

Taarifa ya Ikulu imesema Rais Trump ameridhia kujiuzulu kwa Price na tarifa hiyo kuainisha kwamba Don J Wright atakaimu nafasi hiyo kwa sasa Wright ni Naibu Waziri wa Afya katika serikali hiyo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad