Breaking News: Meneja wa Peacock Hoteli Akamatwa na Polisi kwa Kuhamasisha Ushoga


Breaking News: Meneja wa Peacock Hoteli  Akamatwa na Polisi kwa Kuhamasisha Ushoga
Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Polisi Dar es salaam Lazaro Benedict Mambosasa ambae ametangaza kukamatwa kwa Meneja wa Hoteli ya Peacock Dar es salaam.

“Tumewakamata Wahalifu wengine wa aina yake pale Peacock ambao wanahamasisha ushoga hapa nchini, Wahusika hao kuna raia wa South Africa, Waganda na Watanzania”

“Kwa Tanzania kuna sheria ya kuzuia watu wa jinsia moja kufanya tendo hilo, kwanza Meneja wa Peacock tumemkamata kwa ajili ya kumuhoji, alikua anafahamu ndio maana akatoa ukumbi lakini pia Wahusika hao warudi South Africa wakaendelee huko kama sheria zao zinaruhusu”


“Niliowakamata ni 12, raia wawili wa South Africa, Mganda mmoja na 9 ni Watanzania wenyeji ambao wametoka maeneo mbalimbali… niombe Watanzania kama walivyofanya pale Peacok waendelee kutuamini kwa kutoa taarifa ili tuweze kushughulika nao kwa wakati”

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hebu tuwekee namba zako Mzee Mambo na za kamanda Ciro, mbona mtafurahi

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad