CHADEMA 'wacharuka' kuhusu Mange Kimambi Wamtaka IGP Sirro Kupambana na Wahalifu na Sio Wakosoaji Serikali

Mbunge wa Tarime Vijijini , John Heche amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro kutangaza kiama kwa wahalifu wa wanaofanya mauaji  kwa kupiga watu risasi siyo na siyo kuwatangazia wakosoaji wa Serikali.

Heche amelazimika kusema hayo baada ya hivi karibuni IGP Sirro alipokuwa mkoani Iringa kusema kwamba anafahamu makosa ya mtandaoni yanayofanywa na Mange Kimambi na kuahidi kwamba watamshughulikia.
"IGP anapaswa kuwatangazia kiama wahalifu na watu wanaofanya vitendo vya kupiga watu risasi& kutupa wengine baharini sio wakosoaji wa serikali"

Aidha Kiongozi mwingine wa Chadema aliyeingilia kauli ya IGP Sirro kuhusu Mange Kimambi ni Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ambaye yeye alsema,
"IGPSirro shughulika na usalama wa  raia, malizia uchunguzi BenSanane, TunduLissu na maiti zinazookotwa baharini. Achana na Mange Kimambi"
Hivi karibuni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro alisema kuwa jeshi la polisi linatambua makosa ya kimtandao yanayofanywa na mwanadada Mtanzania Mange Kimambi aishiye nchini Marekani na kusema kuwa jeshi la polisi linashughulikia suala hilo


Kupata Matamko ya Wanasiasa Kila Siku Download App ya Mchambuzi Kwenye Simu yako HAPA
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kama ndio nyinyi mnaemtuma na kumtumia kutukana watu hovyo-hovyo, jasho la meno litawatoka - HACHOMOKI hata mseme kwa kutumia mi....ndu yenu ...msonyooooooooo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad