Haya Ndiyo Maneno ya Nape kwa Tundu Lissu 'Mjomba Tunashukuru Mungu kwa Tabasamu Usiseme Mengi Tulia Mjomba Upone Kabisa '

Haya Ndiyo Maneno ya Nape kwa Tundu Lissu 'Mjomba Tunashukuru Mungu kwa Tabasamu Usiseme Mengi Tulia Mjomba Upone Kabisa '
Mbunge wa jimbo la Mtama kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Nape Nnauye amefunguka na kusema amefurahi kumuona Tundu Lissu akiwa katika furaha na tabasamu na kumuomba kwa sasa asiseme lolote mpaka pale atakapona kabisaa.

Nape Nnauye amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter na kusema tabasamu la Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akiwa kwenye hospitali jijini Nairobi linatoa matumaini makubwa.
"Mjomba tunamshukuru Mungu kwa tabasamu hili la matumaini!Nakuombea afya iimarike kabla hujasema mengi! Tulia mjomba upone kabisa kwanza" alisema Nape Nnauye

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu alishambuliwa na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma nyumbani kwake na baadaye alipelekwa jijini Nairobi kwa matibabu zaidi ambapo mpka sasa anapatiwa matibabu huko.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad