Nyota ya Zari Yazidi Kung'aa Apata Shavu Nono Mercedez- Benz

Nyota ya Zari Yang'aa  Apata Shavu Nono Mercedez- Benz
Mwanadada Zarina Hassan maarufu kwa jina la Zarithebosslady amepata dili la kuonyesha magari aina ya Mercedez-Benz ya kampuni ya AMG Performance Centre iliyoko nchini Afrika ya Kusini.

Hayo yameonekana baada ya mwanadada huyo kuweka picha katika ukurasa wake wa Instagram gari nyeupe aina ya Mercedez-Benz huku akiwa amevalia suti yenye rangi ya zambarau.

Katika kurasa huo aliweka picha tofauti tofauti na kuandika maneno yafuatayo ‘amgperformancecentremenlyn is your centre for class & #stateTheArt cars. Thank you for the car’ na nyingine akiweka #closeDealsInHeels.

Baada ya ujumbe huo mashabiki wake wamempongeza kwa hatua hiyo hasa baada ya yote aliyoyapitia katika maisha yake ya mahusiano na msanii Naseeb Abdul maarufu kwa jina la Diamond Platnumz.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad