Peter Okoye wa P-Square Asaini Mkataba Mnono na Kampuni ya Marekani

Peter wa P-Square Asaini Mkataba Mnono na Kampuni ya Marekani
Peter Okoye maarufu kama Mr P, kutoka kundi la P-Square amesaini mkataba na kampuni ya usambazaji wa muziki ya Empire kutoka Marekani.

Neema hiyo imemdondokea msanii huyo baada ya hivi karibuni kuibuka kwa tetesi za kuvunjika kwa mara ya pili kwa kundi lao la muziki ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu walipoliunda tena baada ya kuvunjika mwaka jana.

Msanii huyo ameonyesha kufurahia hatua hiyo kwa kuandika kwenye mtandao wake wa Instagram, “Thank you Lord🙏🏽😇 RepostBy @empire: “Just had a digital distribution deal with @peterpsquare! Welcome to the #EMPIRE family!” (via #WhizRepost @AppsKottage).”

Kampuni ya Empire ambayo makao yake makuu ni San Franciscomjini California, inafanya kazi na wasanii wakubwa kama Kendrick Lamar pamoja na makampuni mengine makubwa duniani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad