Rais Magufuli Kutoshiriki Kumbukumbu ya Baba wa Taifa


Rais Magufuli Kutoshiriki Kumbukumbu ya Baba wa Taifa
Taasisi mbalimbali za umma na zisizo za umma zinazomualika Mhe. Rais katika shughuli za kumbukumbu ya Mwl. Julius Nyerere zinakumbushwa kutokutangaza ushiriki wa Mhe. Rais Magufuli katika shughuli zao mpaka zipate uthibitisho kutoka Ofisi ya Rais.

Taarifa iliyotolewa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais imesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli hatakuwa mgeni rasmi katika kongamano la maadhimisho ya kumbukizi ya Mwalimu Nyerere kama inavyotangazwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Aidha taarifa hiyo imeongeza kwamba Oktoba 11, 2017 ambayo inatangazwa kuwa ndio siku ya kufanyika kwa kongamano hilo, Mhe. Rais atakuwa na majukumu mengine ya Kitaifa kulingana na ratiba yake ya kazi na kuwataka watu wote kuzingatia utaratibu.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad