RC Makonda Atoa Agizo kwa Jeshi la JWTZ Kujenga Daraja Lililosombwa na Maji Kawe

RC Makonda Atoa Agizo kwa Jeshi la JWTZ Kujenga Daraja Lililosombwa na  Maji Kawe
MKUU wa Mkoa wa Dar es Saalam, Paul Makonda, ametembelea daraja lililokatika Kawe, na kuwapa pole wananchi wa eneo hilo kutokana na athari na hasara walizozipata kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea jijini Dar.
Aidha Makonda amewasihi wananchi waishio maeneo hatarishi kuhama haraka iwezekanavyo, ili kunusuru maisha yao, wasinga’nga’nie kulinda Tv wakati maisha yao yako hatarini.
Katika hatua nyingine Makonda amewaagiza Jeshi la Wananchi Tanzania [JWTZ] Kujenga daraja la muda katika eneo hilo ili kupunguza usumbufu na kuwarahisishia wananchi waweze kutembea kutoka sehemu moja kwenda nyingine, huku mamlaka inayohusika na barabara TAMROADS Wakiendelea na ujenzi wa muda mrefu.
Chanzo Global Publishers
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad