Simbeye Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali ya Gari

Simbeye Anusurika Kifo Baada ya Kupata Ajali ya Gari
Katibu Mwenezi wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), Edward Simbeye amepata ajali ya gari.

Simbeye alikuwa akitokea Dar es Salaam kwenda Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano asubuhi, Simbeye amesema ajali hiyo ilisababishwa na tairi la mbele kushoto kufyatuka hivyo gari kupoteza mwelekeo na kuanguka kando mwa barabara eneo la Kawawa mjini Moshi.

“Namshukuru Mungu nimetoka salama mimi na mdogo wangu… nilikuwa nakwenda nyumbani kwa sababu za kifamilia,” amesema Simbeye.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad