Uingeleza Yaanza kwa Mbwebwe

Uingeleza Yaanza kwa Mbwebwe
Baada ya kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi timu ya taifa ya England imethibitisha kuwa na mechi za kujipima uwezo mwezi Novemba dhidi ya Ujerumani na Brazil.

England imefuzu jana usiku kutoka Kundi F bara la Ulaya baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Slovenia. Timu hiyo imefikisha alama 23 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote kutoka kundi hilo hata akipoteza mchezo wa mwisho na timu zingine zikashinda.
Baada ya kufuzu chama cha soka nchini humo FA asubuhi hii kimethibitisha kuwa timu yao itacheza michezo ya kujipima uwezo dhidi ya timu za Ujerumani na Brazil ambazo nazo zimefuzu kucheza fainali hizo.

Mchezo kati ya England na Ujerumani utachezwa Novemba 10 kwenye uwanja wa Wembley. Baada ya hapo timu hiyo itacheza na Brazil siku nne baadae kwenye uwanja huo huo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad