Dkt Shika Atii Amri ya Polisi Aripoti Kama Kama Alivyotakiwa

Dkt Shika Atii Amri ya Polisi Aripoti Kama Kama Alivyotakiwa
'Bilionea' Dk Louis Shika aliyeibuka mshindi wa kununua nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi leo Novemba 15  ameripoti kituo kikuu cha Polisi Dar es Salaam kama alivyotakiwa.

Dk Shika ameripoti kama alivyotakiwa jana na Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa mara baada ya kuachiwa kwa kujidhamini yeye mwenyewe.

Kabla ya kwenda kuripoti, Dk Shika ambaye amekuwa maarufu kila anapopita, alipata kifungua kinywa maeneo ya Posta.

Saa 2.24 asubuhi, Dk Shika alikuwa amewasili kituoni hapo na ilipofika Saa 3.36 asubuhi aliondoka na kesho atarejea tena kituoni hapo.

Akizungumza na Mwananchi lililokuwapo tangu anaingia hadi anatoka amesema hana tatizo na ataendelea kuitikia wito wa polisi bila tatizo.
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Dkt Shika.
    Ukisha fanya trnsfer Transaction za Roubles into shillings Na kuanzisha Viwanda Kama vitatu.
    Nakusihi uwe mlipa kodi nzuri Ili TRA wasikufanyie haya ya YONO.
    YONO OYEEEEEE. YONO MBELE....
    DKT SHIKA OYEEEE

    ReplyDelete
  2. Dkt Louis.. Tunakuamini.
    Hizi nyumba Ni lazima uzinunue.
    Hela zako za kule Spain zimeshaingia? Na za Bolivia zinakuja Sweden wanasen
    Ma Hujatoa agizo la transfer.
    FANYA KWELI DKT

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad