Farid Musa kuikosa Taifa Stars vs Benin Kutokana na Tatizo la Goti

Farid Musa kuikosa Taifa Stars vs Benin Kutokana na Tatizo la Goti
Ikiwa imepita siku moja tu toka jopo la madaktari club ya KRC Genk ya Ubelgiji inayochezewa na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samatta, watoe taarifa kuwa Mbwana Samatta hatokuwa uwanjani hadi mwanzoni mwa kipindi cha majira ya baridi kufuatia kuumia kwa goti lake la kulia.
Leo taarifa mpya zimetolewa kuhusiana na mtanzania Farid Musa anayecheza soka la kulipwa nchini Hispania akiichezea Tenerife B, Farid Musa ambaye jina lake lilikuwa sehemu ya kikosi cha Taifa Stars kitakachocheza dhidi ya Benin November 12 2017, zimetoka taarifa kuwa ameumia goti.
Farid Musa anaripotiwa kuwa ameumia ligament za goti na anasubiri kufanyiwa vipimo vya mwisho ambayo vitatoa taarifa rasmi kuhusu muda atakaokaa nje staa huyo wa Tanzania lakini taarifa za awali zinaelewa kuwa kwa mujibu wa jeraha lake anaweza kukaa nje ya uwanja kwa kipindi chote cha msimu kilichosalia.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad