Marufuku Kumuweka Mwanangu Kwenye Mitandao ya Kijamii- Masogange

Marufuku Kumuweka Mwanangu Kwenye Mitandao ya Kijamii- Masogange
MREMBO aliyejipatia jina kubwa kutokana na kazi yake ya kuuza nyago kwenye video za wanamuziki Bongo, Agness Gerald ‘Masogange’ amesema kuwa, kwa upande wake ni marufuku kumuweka mtoto wake kwenye mitandao ya kijamii.

Masogange aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, ni bora yeye akiwa anatukanwa na kuambiwa maneno machafu kuliko mwanaye kwa sababu kwenye mitandao watu hawaangalii kama ni mtoto, bali wao ni kutukana tu.

“Siwezi kumnadi mwanangu, ni jambo ambalo nimejiwekea, kama atapenda mambo ya mtandaoni, akija kuwa mkubwa, atajiachia mwenyewe,” alisema Masogange ambaye mtoto mwanaye huyo wa kike ana umri miaka nane sasa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad