Maxence Melo: Rais Magufuli Anafanya vyema Katika Mapambano dhidi ya Ufisadi Lakini Tunahitaji Taasisi imara

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo akihojiwa na vyombo vya Reuters na Sauti ya Amerika(VoA) amesema Serikali ya Rais Magufuli imeonesha dhamira ya kisiasa ya kupambana na vitendo vya ufisadi na rushwa vilivyokuwa vimekithiri nchini lakini akataadharisha bila taasisi imara vita hii inaweza kukwama.

Maxence ameyasema hayo jana katika mahojiano ambayo FikraPevu pia ilikuwepo baada ya kumalizika kwa mdahalo wa kwanza wa Demokrasia Yetu ulioandaliwa na Asasi ya Kiraia ya Twaweza.

Amesema rushwa na ufisadi viliichafua nchi na ilifika wakati hadi watanzania wakaaminishwa kuwa kuna watu hawagusiki lakini tangu Rais Magufuli na Serikali yake waingie madarakani hali imekuwa tofauti kitu ambacho kimepelekea hata tafiti za Twaweza kuonesha kuwa wananchi wanaona kinachotokea kuwa kitu kizuri na cha kupongezwa.

Katika mahojiano hayo, mwandishi alitaka kujua hali ya vitendo vya kifisadi na rushwa nchini na hatma ya uhuru wa kujieleza na vyombo vya habari chini ya Serikali ya awamu ya tano.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad