Ruge Uso kwa Uso na Makonda Kuhusu Tamasha la Fiesta

Ruge Uso kwa Uso na Makonda Kuhusu Tamasha la  Fiesta
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Jumatatu hii amefunguka kuzungumzia tetezi ya kwamba Tamasha la Muziki la Fiesta litaishia 6 usiku tofauti na miaka iliyopita kutokana na hali ya usalama.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda hivi karibuni akiwa katika kituo cha redio cha EFM kuzungumza juu ya matukio ya burudani kutotakiwa kufanyika zaidi ya saa sita usiku kwenye maeneo ya wazi Dar es salaam.

Tamasha la FIESTA 2017 linatarajiwa kufanyika Leaders Club Jumamosi hii November 25 huku ticket tayari zikiwa zimeshazagaa mitaani.

Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group amesema “Tunafanya juhudi za kujaribu kuona kama tunaweza tukampata Mkuu wa Mkoa”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad