Ujumbe wa Nape Nnauye Baada ya Nyalandu Kujiuzulu' Chama Cha Siasa Ni Itikadi'

Ujumbe wa Nape Nnauye Baada ya Nyarandu Kujiuzulu' Chama Cha Siasa Ni Itikadi'
Baada ya Mbunge wa Singida Kaskazini kujivua ubunge na kujiondoa katika chama cha Mapinduzi(CCM), Lazaro Nyalandu hatimae Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema kuwa Chama cha siasa ni Itikadi.

Nape kupitia ukurasa wake wa twitter ameweka picha inayomuonyesha mbunge huyo na Katibu Mkuu wa Chama hicho, Ndg Kinana wakiwa wameweka kwa pamoja alama ya kidole gumba.

Chama cha siasa ni ITIKADI, itikadi ni IMANI.Siamini SANA katika kubadili Imani KIENYEJI.Nitashughulikia MAPUNGUFU nikiwa ndani sio NJE!

Nyalandu alikihama chama cha Mapinduzi Oktoba 30 mwaka huu ambapo alieleza kuwa amechoshwa na mwenendo wa siasa wa sasa.


Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad