Zuma: Nimewasiliana na Mugabe na Yuko Salama

Zuma: Nimewasiliana na Mugabe na Yuko Salama
Rais Robert Mugabe "yuko salama", rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema.

Bw Zuma amesema amezungumza na kiongozi huyo wa miaka 93 kwa njia ya simu.

Amesema Mugabe amemjulisha kwamba yupo nyumbani kwake ambapo amezuiwa kuondoka, kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka kwa afisi ya rais wa Afrika Kusini.

Zuma amesema kwamba amewasiliana pia na Majeshi ya Ulinzi ya Zimbabwe (ZDF), taarifa hiyo imesema.

Afrika Kusini inapanga kuwasiliana na pande zote mbili.

Bw Zuma amekariri wito wake wa awali kwamba kuwe na "utulivu"
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad