CHADEMA chawataka wabunge wake kujiondoa michuano ya mabunge EAC

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeazimia kuwa wabunge wake wote wanaoshiriki Michezo ya Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanatakiwa kuondoka mara moja kwenye kambi ya timu ya Tanzania.

CHADEMA kimefikia uamuzi huo katika kikao chake cha dharura kinachoendelea ambacho kiliitishwa kwa lengo la kutafakari kwa kina maendeleo ya hali ya siasa nchini.

Chama hicho kimesema kuwa maagizo hayo yameanza kutekelezwa usiku wa Jumatano, Disemba 6 mwaka huu baada ya kupitishwa kwa azimio hilo ambapo Kamati Kuu ilimuagiza Katibu wa Bunge kuwafikishia wabunge wahusika mara moja

Baada ya kupokea tathmini ya kina ya Uchaguzi wa marudio katika Kata 43 uliofanyika hivi karibuni CHADEMA kimebaini kuwa ulitawaliwa na uvunjifu Mkubwa wa Haki za binadamu.

Aidha CHADEMA kimesema kuwa maazimio mengine ya kikao cha Kamati Kuu ambacho kinaendelea jijini Dar yatatolewa katika hatua ya baadae ambapo umma utaarifiwa rasmi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad