Chadema Wamteua Patrick Sosopi Kurithi Nafasi ya Katambi

Chadema Wamteua Patrick Sosopi Kurithi Nafasi ya Katambi
BARAZA la Uongozi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamefanya uteuzi wa viongozi wa Baraza la Vijana la Chama hicho (BAVICHA) ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi kufuatia baadhi ya viongozi wao kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi hivi karibuni.
Katika uteuzi huo, Balaza hilo limemteua aliyekuwa Katibu wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi kuwa Mwenyekiti mpya wa BAVICHA, baada aliyekuwa mwenyekiti wa baraza hilo, Patrobas Katambi kuhamia CCM. Ole Sosopo ataitumikia nafasi hiyo kwa muda wa mwaka mmoja kabla ya uchaguzi kufanyika mwakani 2018.
Aidha, chama hicho kimemteua ndugu Pambalu kuwa katibu wa Bavicha baada ya nafasi hiyo kuachwa wazi na Ole Sosopi aliyeteuliwa kuwa mwenyekiti wa muda.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad