CUF Inayomuunga Mkono Lipumba Yafunguka Kuhusu Kuhama kwa Mtulia

CUF Inayomuunga Mkono Lipumba Yafunguka Kuhama kwa Mtulia
CHAMA cha Wananchi upande wa Prof. Ibrahim Lipumba, leo Desemba 4, 2017 kimetoa ufafanuzi huu aliekuwa Mbunge wa Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia aliyejivua uanachama na kuachia ngazi nyadhifa zote ndani ya chama hicho huku akitangaza kuhamia CCM.
CUF imefunguka leo ikiwa ni siku moja tangu Mtulia atangaze uamuzi huo juzi ambapo alisema ameridhishwa na utendaji wa Rais Magufuli hivyo haoni haja ya kuendelea kuwa mpinzani hivyo ni bora akamuunga mkono Rais.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar, Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma CUF, Abdul Kambaya amesema kuwa Maulid Mtulia ameondoa uaminifu kwa wanachama wa Jimbo la Kinondoni kwa madai ya kuwa wananchi walimwamini kulala nje wakipigania kula zake za ubunge huku wengine wakiumizwa na kufikishwa mahakamani lakini yeye amewasaliti.
Amesema kuwa Mtulia amekitia doa chama chao kutokana na matande yake aliyoyafanya kwa wananchi na chama kwa ujumla huku akisema kuwa kuhama kwake chama kwa madai yakuwa nikutokana na kwamba anamuunga mkono Rais hazina mashiko hata kidogo.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Bora mtulia msaliti lakin si mnafki kama wewe kambaya

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad