Kisa Kuolewa na 'Kiben Ten' Mama Mobeto Ampa Makavu Mama Daimond

Kisa Kuolewa na 'Kiben Ten' Mama Mobeto Ampa Makavu Mama Daimond
MAMA mzazi wa Mwanamitindo maarufu Bongo Hamisa Mobeto, Shufaa Lutigunga amefunguka kuwa hayuko tayari kuolewa na “Serengeti Boy” wakati watu wazima wenzie wapo, kitendo ambacho kimetafsiriwa kuwa ni kumchana mama Esma.

Akizungumza na Risasi Jumamosi Mama Mobeto alisema kuwa, sasa hivi ameshakuwa mtu mzima na ni bibi mwenye wajukuu hivyo kuolewa na kijana mdogo ni kujishushia hadhi kama mama na bibi pia.

“Jamani mimi kama ni kuolewa basi nitaolewa na mtu mzima mwenzangu kwasababu Serengeti Boy kwangu haiwezekani, nahitaji kuolewa kweli ila nitaolewa na mzee mwenzangu ili wajukuu wapate babu,” alisema Mama Mobeto ambaye kwa kuongea hayo ni kama amemchana mama Esma amefunga ndoa hivi karibuni na kijana anayedaiwa kuwa ni Serengeti Boy kwake

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad