Leo Tanzania Yaadhimisha Miaka 56 ya Uhuru

Leo Tanzania Yaadhimisha Miaka 56 ya Uhuru
Leo, Disemba 09, 2017 Tanzania inaadhimisha miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara (Tanganyika) ambapo sherehe hizo zinafanyika katika Uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.
Katika Maadhimisho hayo ya Uhuru wa Tanzania Bara, Rais Dkt. ndiye Mgeni Rasmi. Viongozi wengi wameshawasili katika viwanja hivyo kwa ajili ya kujumuika na Watanzania wengine kusherehekea.
Kikosi cha Jeshi la Wananchi Tanzani (JWTZ) na vikosi vingine vya ulinzi wanapita mbele ya Rais na Amri jeshi Mkuu kutoa salam zao za heshima kwa mkuu huyo wa nchi.
Sherehe hizi zinaadhimishwa huku kukiwa na simanzi kitaifa kufuatia askari wetu wanaolinda amani DRC kuuawa na wengine kujeruhiwa vibaya kufuatia shambulizi lililofanywa na waasi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad