Lusekelo Atoboa Siri Chanzo cha Kuvunja Ndoa za Watu

Lusekero Atoboa Siri Chanzo cha Kuvunja Ndoa za Watu
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini DSM, Lusekelo 'Mzee wa Upako' amefunguka na kusema kuwa wachungaji wengi wanavunja ndoa za watu hasa pale inapofahamika kuwa mwanaume anatatizo la nguvu za kiume au mwanaume kupenda mtelezo.


Mchungaji Lusekelo alisema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na mtangazaji Joyce Kiria kwenye kipindi cha WANAWAKE LIVE na kusema kuwa wachungaji wengi wamekuwa wakivunja ndoa za wanandoa wengi ambao wanaume wanakuwa wamebainika kuwa na tatizo la nguvu za kiume.

"Sisi kuna kesi nyingi tumepata mfano watu walioana kumbe mwanaume hawezi tendo la ndoa, wachungaji ndoa za namna hii wanavunja nyingi tu, kwamba huyu bwana hawezi na hana nguvu za kiume wanavunja kabisa. Lakini pia yule mkatili kabisa kabisa anachengua watoto, hasomeshi watoto" alisema Mchungaji Lusekelo
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad