Nyota wa Mpira, Emmanuel Eboue Atamani Kujiua Baada ya Kufilisiwa na Mwanamke

Staa wa soka wa kimataifa wa Ivory Coast aliyewahi kuvichezea vilabu mbalimbali Ulaya kama Arsenal na Galatasaray ya Uturuki Emmanuel Eboue amedai  kufilisika  baada ya talaka, iliyompa mali zote mkewe Auerilie Bertrand

Eboue kwa sasa ana umri wa miaka 34 na anaitumikia adhabu ya kufungiwa mwaka mmoja na FIFA kwa kushindwa kumlipa wakala wake.

Eboue licha ya kutokea katika maisha magumu Ivory Coast alifanikiwa kutengeneza pesa nyingi akiwa katika Ligi Kuu England akiitumikia Arsenal kwa miaka saba.

Beki huyo wa zamani wa Arsenal kwa sasa yupo katika maisha magumu na analala chini kwa rafiki yake huku akishindwa kulipia pesa nguo zake ziende dry cleaner, hivyo analazimika kufua kwa mikono. Eboue anatajwa kuelekea kufilisika kutokana na kutalakiana na mkewe.

Hali hiyo imemfanya Eboue kuwa masikini  kutokana na utajiri wake wote kumuandikisha mkewe.

Kisheria wakiachana mali zote zitakuwa za mwanamke ambaye amezaa nae watoto watatu, jambo ambalo Eboue linamfanya aumie kichwa na kuweka wazi kuwa mara kadhaa linamjia wazo la kujiua kichwani kwake na anaomba Mungu aliepuke.

 Eboue ameichezea Arsenal kwa miaka saba kabla ya mwaka 2011 kuamua kujiunga na Galatasaray ya Uturuki.

“Pesa zote ambazo nilikuwa naingiza nilikuwa natuma kwa mke wangu kwa ajili ya watoto wetu, nikiwa Galatasaray Uturuki nilikuwa naingiza euro milioni nane na nilikuwa namtumia euro milioni 7, chochote alichokuwa anataka nisaini nilikuwa nasaini”-Eboue
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ndipo ulipo udhaifu wa kiumbe aitwae mwanamke!
    Hatari sheikh hasa huku dunia ya 3 ambako wamempa mwanamke uhuru kupindukia.
    Utashangaa baadhi yao wanavokosa huruma.
    Mitihani ya dunia!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad