Rais Ali Mohammed Shein Akunwa na Zanzibar Heroes..Awapa Zawadi Kem Kem


Rais Ali Mohammed Shein amewapa zawadi ya Shilingi milioni tatu na kiwanja kimoja kwa kila mchezaji wa Timu ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes aliyeshiriki mashindano ya CECAFA yaliyomalizika nchini Kenya na Zanzibar kushika nafasi ya pili.


Rais huyo ametoa wito kwa Wazanzibari kuipenda timu yao kwani hakuna atakayeipenda kama wao hawaipendi na kutolea mfano wanaitwa urojo ila hawawezi kuendelea kuitwa urojo tena.

Rais Shein pia amewataka Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kuacha kupeleka masuala ya mpira mahakamani kwani ni kinyume na kanuni za FIFA na inaitia aibu Zanzibar.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad