Rais wa Zimbabwe Kuteta na Zuma Afrika Kusini

Rais wa Zimbabwe Kuteta na Zuma Afrika Kusini
Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe amefanya ziara ya kwanza nje ya Taifa tangu aapishwe mwezi uliopita kwa kutembelea Afrika Kusini.

Msemaji wa Rais, Bongani Ngqulunga amesema Mnangagwa leo Alhamisi Desemba 21,2017 atamtembelea Rais Jacob Zuma mjini Pretoria.

Viongozi hao wawili watazungumzia masuala muhimu ya maendeleo ya kikanda, Bara la Afrika na kimataifa.

Kwa mujibu wa ubalozi wa Zimbabwe nchini Afrika Kusini, Rais Mnangagwa anatarajiwa kutumia fursa hiyo kuvutia uwekezaji kutoka nchi hiyo jirani.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad