Timu ya Bunge Yaichapa Kenya Bao 1-0

Timu ya mpira wa miguu ya Bunge ya Tanzania, imetumia vema uwanja wake wa nyumbani Kwenye mchezo uliopigwa jioni hii dhidi ya Kenya ambapo imeibuka na us ushindi goli 1 - 0 katika michuano ya Wabunge wa Afrika Mashariki inayoendelea hapa nchini.

Mchezo huo  uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa timu ya bunge la Tanzania ilijipatia goli hilo katika kipindi cha pili  huku timu ya bunge la Kenya ikijitahidi kupeleka mashambulizi lakini ikashindwa kurudisha goli hilo.


Katika mechi hiyo ambayo ilikua na upinzani mkali timu ya bunge ya Tanzania iliweza kutawala mchezo kwa kipindi cha kwanza lakini walishindwa kupata goli  huku kipindi cha pili wakionekana Kufanya hivyo  ndipo walipata goli hilo la kuongoza hivyo hadi mwisho wa mchezo Timu ya Bunge ya Tanzania ikaibuka kidedea katika mchezo huo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad