Trump Kuutambua Jerusalem Kuwa Mji Mkuu wa Israel

Mji wa JerusalemTrump Kuutambua Jerusalem Kuwa Mji Mkuu wa Israel
Maafisa wa serikali ya Marekani wamesema kuwa rais Donald Trump, leo atautambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel.
Ikulu ya White House imethibitisha kuwa rais Donald Trump pia atazungumza kuhusu juu ya kutangaza rasmi kuhamishia kwa ubalozi wa Marekani Jerusalem.
Kwa mujibu wa msemaji wa ikulu ya white house sarah sanders amesema kuwa Trump alizungumza na baadhi ya viongozi siku ya jumanne kuhusu mpango yake ya kuhamishia ubalozi huo kutoka Tel Aviv kuupeleka Jerusalem.
Kwa nini mji wa Jerusalem ni mtakatifu?
Jordan yaitaka Marekani isiutambue Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel
''Amezungumza na baadhi ya viongozi asubuhi ya jana na atendelea kuwa na majadiliano na wadau wanaohusika lakini atafanya maamuzi yenye umuhimu kwa Marekani''
Wakati huo huo viongozi wa Palestina, Misri, Jordan na Saudi Arabia, wametoa onyo kwa rais Trump kuwa kuhamishia ubalozi huo Jerusalem kutadhoofisha kabisa juhudi za kuleta amani mashariki ya kati.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad