Waziri Mkuu atoa onyo kali kwa Madiwani

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Madiwani katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma kuachana na makundi yanayoigawa Manispaa hiyo kwani yanakwamisha utekelezaji wa miradi.

Waziri mkuu ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya siku moja katika mkoa wa Ruvuma wakati akizungmza na watumishi pamoja na Madiwani hao ambapo amewaambia kama watashindwa kuzimaliza tofauti zao yeye atawafukuza.

“Madiwani mnaigawa Halmashauri, pamoja na nguvu mliyonayo ya kuiendesha Halmashauri lakini mnaiendesha vibaya, miradi haijengwi vizuri, mmeingiza maslahi binafsi, wakati mwingine pesa zinatumwa mnaanza kubishana tu, sasa ni mwisho mkiendelea tutawafukuza, amesema Waziri Mkuu.

Majaliwa ameongeza kuwa serikali inakusanya kodi ili wananchi wapate maendeleo lakini wao wanachelewesha miradi ya maendeleo kwa malengo ya kuikwamisha Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivyo hatakubali na atawafukuza.

Aidha amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa kazi nzuri anayoifanya na kumtaka kuripoti kwake endapo pesa zitaingia kisha Madiwani kuanza kubishana bila utekelezaji ili awashughulikie hata kama ni Meya wa Manispaa hiyo.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad