Yanga SC Yateua Wanachama 28 Kuunda Kamati Mpya ya Mashindano.

Yanga SC Yateua Wanachama 28 Kuunda Kamati Mpya ya Mashindano.
Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara klabu ya Yanga SC imeteua wanachama 28 kwaajili ya kuunda kamati mpya ya mashindano.

Taarifa ya klabu hiyo imeeleza kuwa kamati hiyo itakuwa chini ya Mwenyekiti Hussein Nyika, Makamu wake Mustapha Ulungo na Katibu Mkuu Samuel Lukumay.

Uteuzi huo umefanyika jana katika kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam huku.

Yanga inakamata nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na pointi 21 baada ya mechi 11, ikizidiwa pointi mbili na vinara Simba na Azam FC.

Yanga itasafiri Desemba 31 hadi jijini Mwanza ambapo itakwaana na Mbao FC kwenye uwanja wa CCM Kirumba, ikiwa ni mwendelezo wa mechi za ligi kuu msimu wa 2017/18.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni kama inavyoonekana hapo chini.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad