Chelsea Yalazimishwa Sare na Arsenal Nyumbani

Chelsea walikuwa nyumbani kuwakaribisha Arsenal katika moja ya mchezo moubwa sana siku ya leo, hadi dakika 90 zinafika timu hizo zilitoshana nguvu ya bila kufungana.

Sare ya leo inazifanya timu hizo mbili kutoka sare mara nne katika msimu mmoja wa ligi idadi kama hii ya sare mara ya mwisho ilitokea ilikuwa msimu wa 2002/2003 kati ya Blackburn na Sunderland.

Katika mchezo huo kama kawada kiungo wa klabu ya Arsenal Jack Wilshere aliumia tena haki iliyoleta hofu kwa mashabiki lakini daktari amesema bado wanaendelea kumpima kujua kama atakuwa nje kwa muda au laa.

Mchezo wa leo pia ulimfanya Francis Coquelin kuwa mchezaji anayecheza ndani ya uwanja aliyecheza michezo mingi bila kuifungia  Arsenal goli, sasa nusu fainali hiyo ya EFL intarajiwa kwenda kurudiwa Emirates hapo baadaye.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad