Cilic Atinga Fainali Baada ya Kumchapa Mpinzani Wake Kyle Edmund

Cilic Atinga Fainali Baada ya Kumchapa Mpinzani Wake Kyle Edmund
Mcheza tenisi kutoka nchini Croatia, Marin Cilic amefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali baada ya kumchapa mpinzani wake Kyle Edmund katika hatua ya nusu fainali.

Cilic amefanikiwa kutinga katika hatua hiyo kwa ushindi wa seti 6-2 7-6 (7-4) 6-2.

Kutokana na ushindi huo, Cilic anaweza kupanda mpaka nafasi ya tatu katika viwango vya ubora wa mchezo huo duniani vitakavyotoka wiki ijayo.

Kwa sasa mchezaji huyo ana subiri kucheza fainali na mshindi wa mchezo kati ya Roger Federer na Hyeon Chung ambao watachuana kesho (Ijumaa).

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad