Dudu Baya Awachana Basata

Dudu Baya Awachana Basata
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Dudubaya amesema hajapendezwa na tabia ya Baraza la Sanaa Tanzania la kufungia fungia kazi za Wasanii kwa vigezo vya kukiuka maadili.

Dudubaya amedai BASATA wamekuwa wakifungia kazi za wasanii ambazo tayari zimeshatoka na zimeanza kutumika kitu ambacho kinaonekana kama msukumo kutoka kwa watu.

Dudubaya amesema BASATA wamekuwa wakitoa maamuzi hayo kwa kukurupuka na sio kwa kufuata taratibu kama inavyotakiwa.

Kwa upande mwingine Dudubaya ameweka wazi msimamo wake kuhusu  utawala wa Rais Magufuli, ambapo amesema anapendezwa na maamuzi yake ya kuzuia wasanii wa kike kuvaa nguo za ajabu kwenye video.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad