Faida na Hasara Zampa Kigugumizi Harmorapa

Faida na Hasara Zampa Kigugumizi Harmorapa
Msanii wa muziki anayefanya vyema katika mitandao ya kijamii hasa Instagram, Harmorapa amejikuta akipata kigugumizi kuhusu kuingiza faida au hasara katika menejementi yake Sabuka Music.

Akiongea na Bongo5 msanii huyo anayehit na ngoma kadhaa kama vile ‘Shindu’ na ‘Mr.Kiki’ amedai kuwa yeye hafahamu kama ameingiza hasara au faida alipokuwa Sabuka Music.

“Baada ya Mr. Kiki kuna kazi zinakuja nitandondosha mzigo baada ya mzigo, harafu kwanza sipo katika menejiment mpya nafanya kazi zangu mimi kama mimi” amesema msanii huyo baada ya kuulizwa kama yupo katika manejement mpya.
Harmo akaongeza kuwa ni mpiango ya kazi tu kufanya kazi mwenyewe kwani ni jambo la kawaida ku-move kutoka hapo kwenda sehemu nyingine.

“Mimi nikizungumzia sana hapo kuhusu kama kuna faida ama hakuna faida hapo mimi sijui kiufupi yani. Nisema imeingiza faida hapo ama sijaingiza faida yoyote kipindi ambapo nipo sabuka muziki” Amesisitiza msanii huyo baada ya kuulizwa kuwa kuna tetesi kuwa amaingizia hasara menejimenti yake ya Sabuka.

Kuhusu kuhusika katika sakata la kumfukuzisha msanii mwezake katika menejimenti hiyo Harmo amedai kuwa yeye hakuhusika kumfukuzisha Kiloriti ila alikuwa na mambo yake.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad