Hii ndio Benki Mpya iliyopewa Leseni ya Biashara na Benki Kuu ya Tanzania

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa taarifa kwa kwa umma kuwa, imetoa leseni ya biashara kwa benki mpya yenye jina, Guaranty Trust Bank (Tanzania) Limited.

Leseni hiyo inatoa kibali kwa taasisi hiyo kutoa huduma za kibenki nchini Tanzania kama benki ya kibishara na imetolewa kuanzia Januari 5, 2018.

Makao Makuu ya Benki hiyo yanapatikana Kitalu namba 4, Regent Estate, Barabara ya Bagamoyo, jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ya Benki Kuu imekuja siku chache tangu ilipozifutia leseni za biashara, benki 5 ambazo ni Covenant Bank, Efatha Bank, Njombe Community Bank, Kagera Farmers’ Cooperative Bank, na Meru Community Bank.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad