“Jamani Huu Mjadala wa Nguo Fupi… Haiwezekani Watu Watembee na Futi Mitaani” – Tibaijuka

Kumekua na mjadala kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii baada ya habari kusambaa kwamba Wanawake wanaovaa nguo fupi na Wanaume wanaovaa milegezo, kunyoa viduku na suruali zilizobana Arusha na Dar es salaam wanakamatwa na Polisi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa alikanusha kuhusu Polisi Dar kukamata wanaofanya hivyo kwa kusema alinukuliwa vibaya.

Sasa baada ya kuona mijadala inaendelea kwenye mitandao ya kijamii, Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amejitokeza na kuongea yafuatayo >>> “Yani kuna vitu vingine huwezi kusema Muafrika alikua anavaa nguo ndefu, hapana sio kweli…”

“Mwili wa Mwanamke unaonekana ni kifaa ambacho Mungu amekiweka kwa shughuli maalum ya Uzazi, Ulezi n.k sasa ambae anajiheshimu anajua nini cha kuvaa katika wakati gani, cha msingi ni maadili ya mavazi na pale ulipo“

“Hiki sio kitu ambacho kitasimamiwa huwezi tena kuwa tena na Watu wanatembea na futi mitaani kupima urefu au ufupi wa nguo, jamanijamani tunazo kazi nyingi za kufanya” – Profesa Tibaijuka …… msikilize zaidi hapa chini
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. U r right mama tibaijuka. Km ni mwafrica tena mfano, ni mwanariadha au muogeleaji kuvaa chupi pale stadium huku maelfu ya watu wakikutazama ni Sawa tu,na heshima ya mttu inabakia vilevile. Ila katika tukio hilo hilo ukivaa suruali au nguo ndefu na viatu virefu na handbag mkononi watu watakunyoshea kilometres. Au ukivaa nguo ya arusi ambayo ni ya heshima na shela lake kwenye bwawa la kuogelea au sokoni au shambani au ofisini, inaweza kuonekana ni kukosa maadili ,

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad