Kocha Zinedine Zidane wa Madrid Adhibitisha Ronaldo Ataendelea Kubaki Madrid


Baada ya kuwepo kwa habari nyingi kuhusu Ronaldo kutaka kuondoka Real Madrid, hatimaye kocha wa mabingwa hao wa Hispania Zinedine Zidane amesema nyota huyo hataondoka.

''Ronaldo kuondoka Madrid ni jambo la kufikirika, siwezi kuifikiria Real Madrid bila Ronaldo, lakini nina uhakika kuwa mpango wa Ronaldo ni kumalizia soka ndani ya klabu hii'', amesema Zidane mchana huu mbele ya wanahabari kuelekea mchezo wa La Liga dhidi ya Celta Vigo.
Zidane amelazimika kuongelea suala hilo baada ya siku za hivi karibuni kuwepo kwa taarifa kuwa nyota huyo wa Ureno anashinikiza kupatiwa mshahara mnono utakao mfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani tofauti na hivi sasa ambapo anazidiwa na mpinzani wake Lionel Messi pamoja na Neymar Jr.
Ronaldo mwenye miaka 32 ambaye pia ni mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo alisaini mkataba mpya mwaka 2016 unaomweka klabuni hapo hadi mwaka 2011.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad