Muna Love Awashawishi Wasanoii Wenzake Kuokoka

Muna Love Awashawishi Wasanoii Wenzake Kuokoka
MSANII wa Filamu za Bongo na mdau wa Muziki wa Bongo Fleva, Rose Alphonce ‘Muna Love’ ambaye aliamua kuokoka baada ya mtoto wake, Patrick kuugua na kupona kimiujiza, amewataka wasanii na wadau wake wamrudie Mungu.

Muna aliiambia Full Shangwe kuwa, ataongea na marafiki zake wakiwemo Wakristo na Waislamu wamrudie Mungu kwani kupona kwa mwanaye ni uwezo wa Mungu.

“Ninawaomba marafiki zangu wote wanaonizunguka kumrudia Mungu kwa imani zao. Mimi nimemuona Mungu baada ya kumponya mwanangu kimaajabu. Patrick aliniomba nimuitie mchungaji ili amuombee, nilishangaa kwa imani kali aliyonayo kumbe Mungu aliamua kumtumia ili niokoke.

“Kwa sasa ninaabudu Doricas Ministry iliyoko Kunduchi jijini Dar, ninajipanga kulitangaza neno la Mungu,”alisema Muna.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad