Mwizi Baada ya Kukusanya Vitu Alivyotaka Kuiba Apitiwa na Usingizi Alala Kwenye Kochi

Mwizi Baada ya Kukusanya Vitu Alivyotaka Kuiba Apitiwa na Usingizi Alala Kwenye Kochi
Hivi karibuni jeshi la Polisi nchini Ujerumani katika ukanda wa kati limemtia mbaroni mwanaume mmoja mwizi ambaye aliingia kwenye nyumba moja, akiwa na dhumuni la kuiba lakini baada ya kukusanya vitu anavyotaka kuondoka navyo, akapitiwa na usingizi kwenye sofa la ndani ya chumba cha mazoezi ya yoga katika nyumba hiyo.

Ilipofika asubuhi wenyeji wa nyumba hiyo walikuta mwizi huyo amelala kwenye kochi lao na vitu alivyotaka kuiba vikiwa tayari vimefungashwa na ndipo walipotaarifu polisi kuhusu tukio hilo.

Taarifa ya polisi ilieleza kuwa mwanaume huyo wa miaka 40 aliingia kwenye nyumba hiyo usiku akitaka kuiba na kueleza kuwa inawezekana alikuwa ametumia dawa za kulevya jambo lililomfanya ashindwe kutoka badala yake alale usingizi kwenye kochi hilo.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad