Salum Mwalim Ajiweka Mguu Sawa Kupambana Vikali na CCM Ubunge Kinondoni


Mgombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA katika Jimbo la Kinondoni, Salum Mwalim Juma amerudisha fomu ya kugombea Ubunge Jimbo hilo

Fomu ya Mgombea huyo ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa Upande wa Zanzibar imepokelewa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni Bi. Latipha Ramadhani Almas

Jimbo la Kinondoni lilitangazwa kuwa wazi na Tume ya Uchaguzi (NEC) baada ya aliyekuwa Mbunge wake kupitia chama cha CUF, Maulid Mtulia kujiuzulu na kuhamia CCM

Salum Mwalimu pamoja na Wagombea wa Vyama vingine watachuana na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo ambaye ameipitishwa na CCM kugombea tena nafasi hiyo
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad