Snura Afunguka Skendo ya Kukwapua Bwana wa Nisha

Snura Afunguka Skendo ya Kukwapua Bwana wa Nisha
MSANII wa filamu Bongo, Snura Mushi amefungukia uvumi wa kumkwapua bwana aliyekuwa anatoka na msanii mwenzake, Salma Jabu Nisha aitwaye Minu na kusema kuwa, jamaa
huyo ni mtu wake wa karibu tu siyo kimapenzi.

Balaa hilo liliibuka siku chache zilizopita kwenye mitandao ya kijamii baada ya msanii huyo kumtakia heri ya kuzaliwa Minu kwa maneno matamu ambayo watu walianza kujaji kuwa huenda ni wapenzi, ambapo alifunguka kuwa hana uhusiano na mwanaume huyo kwani ukaribu wao ni wa kikazi si zaidi.

“Huyo Minu siyo mpenzi wangu na wala sina muda mrefu tangu nijuane naye, kuna siku alinitafuta baada ya kupewa namba yangu na Nisha, sababu alikuwa ameandika wimbo ambao aliona nafaa kuuimba, sasa kumtakia heri ya kuzaliwa kwa kumwambia nampenda ndiyo kosa?”alihoji msanii huyo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad