Waombolezaji Watimua Mbio Baada ya Mtu Aliyedhaniwa Amekufa Kuibukia Msibani

Waombolezaji Watimua Mbio Baada ya Mtu Aliyedhaniwa Amekufa Kuibukia Msibani
Wakazi wa kijiji cha Marindi huko Kaunti ya Migori walipaniki na kuchanganyikiwa baada mwanaume wa miaka 35 ambaye aliaminika kuwa amefariki kuibukia msibani nyumbani kwake ghafla

Familia ya mwanaume huyo walikuwa wakimalizia mipango ya mazishi ndipo Okelo Nyamwaga alipojitokeza

Kufika kwake huko kusikotarajiwa kulileta hofu na furaha katika familia yake na marafiki na waombolezaji wengine kukimbia

Nyamwaga alikuwa amepotea kwa miezi miwili na familia yake ilipoteza matumaini ya kumpata akiwa hai

Wiki moja iliyopita marafiki wa Nyamwanga walisema mwili wake ukiwa umeharibika ulikuwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Migori

Mwili huo uliokotwa mtoni ukiwa umeharibika na kupelekwa mochwari
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad