Chama cha ACT- Wazalendo Watoa Taarifa Kufuatia Kifo cha Kingunge

Chama cha ACT- Wazalendo Watoa Taarifa Kufuatia Kifo cha Kingunge
Chama cha cha ACT – Wazalendo kimeeleza kuwa kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mwanasiasa Mkongwe hapa nchini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru kilichotokea usiku wa kuamkia leo katika hopsitali ya Taifa Muhimbili.

Katika taarifa iliyotolewa leo na Chama hicho imeeleza kuwa Mzee Kingunge atakumbukwa kwa mchango wake kwenye mapambano ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Aidha Chama cha ACT Wazalendo wanatoa pole kwa familia ya Mzee Kingunge kwa kupata misiba miwili ndani ya kipindi kifupi Mzee Kingunge aliyefariki usiku wa kuamkia Februari 2, 2018 na Mkewe Mama Peras Kingunge aliyefariki Januari 4, 2018

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad